Winnie Mandela, mke wa zamani wa Nelson Mandela, ambaye pia alipigana dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini amefariki dunia akiwa na miaka 81. Habari za kifo chake zimethibitishwa na msaidizi wake. Winnie alizaliwa mnamo 26 Oktoba mwaka 1936, na ingawa yeye na mumewe – Nelson Mandela – walitalikiana mapema miaka ya 1990, Winnie Madikizela Mandela kama alivyofahamika rasmi alisalia kutoa mchango katika maisha ya Bw Mandela. Alikuwepo na walishikana mikono alipokuwa akiondoka gerezani baada ya kufungwa kwa...
Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa amewaomba viongozi wa dini popote walipo wahakikishe wanaipigania na kuilinda amani kwa kila hali ikiwani pamoja na kupambana na viashiria vya uvunjifu wa amani. Wito huu unatolewa siku chache baada ya baadhi ya makanisa ya kikristo kukosoa utendaji wake. Baraza la maaskofu wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri chini Tanzania (KKKT) kusema kuwa Umoja na amani ya Tanzania viko hatarini. Katika waraka wa ujumbe wa pasaka uliosambaa katika mitandao ya kijamii , baraza hilo...
...
Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar, Zuberi Katwila amejipambanua na amesema wamejiandaa vizuri kuhakikisha leo lazima wawafunge Azam FC na kutinga hatua ya Nusu Fainali Kombe la FA. Mtibwa Sugar inacheza mechi ya robo fainali ya Kombe la FA kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam na Katwila anaamini wamejiandaa hasa. “Azam wana timu nzuri lakini kweli tumejiandaa sana na tuko Dar es Salaam kutafuta matokeo ya mechi hiyo,” alisema. Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na...
Kikosi cha Yanga kesho kitashuka dimbani Uwanja wa Namfua kwa ajili ya kucheza dhidi ya Singida United kutafuta nafasi ya kutinga hatua ya nusu fainali Kombe la FA. Yanga ambayo ilikuwa imeweka kambi ya muda mfupi mjini Morogoro, tayari ipo Singida huku ikielezwa wachezaji wake wote wapo fiti kiafya. Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Yanga, Dismas Ten, amesema wachezaji wote wapo sawa kuelekea mchezo huo, na jukumu limesalia kwa Mwalimu, George Lwandamina, kuamua nani amuanzishe. Singida itakuwa inaikaribisha Yanga...
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limepokea barua kutoka CECAFA ikiomba Tanzania kuwa mwenyeji wa mashindano ya Kombe la Kagame kwa ngazi ya klabu. TFF imepokea barua hiyo leo ikiitaka Tanzania iwe mwenyeji wa michuano hiyo ambayo mara nyingi hufanyika jijini Dar es Salaam inapotokea Tanzania kwa mwenyeji. Kwa mujibu wa Afisa Habari wa TFF, Clifford Mario Ndimbo, amethibitisha shirikisho hilo kupokea barua hiyo na kuahidi kuifanyia kazi. “Ni kweli tumepokea barua ya CECAFA ikiomba Tanzania tuwe wenyeji wa michuano ya...
Mwanza Madereva wa Daladala wanaofanya safari zao Airpot Nyashishi na Kisesa Nyashishi wilayani Misungwi wamelazimika kugoma baada ya Sumatra kuongeza ruti bila kuongeza nauli. Madereva hao wamelalamikia kitendo hicho kwakuwa ruti iliyopangwa sumatra haijatoa bei elekezi nauli itakuwa sh Ngapi, kutokana na umbali. Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza Anthon Bahebe ameliomba Jeshi la Polisi kitengo cha Usalama barabarani pamoja na mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa Majini na nchi kavu sumatra kusimamia suala hilo ili...
Rais wa Marekani Donald Trump amesema leo kuwa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un yuko tayari kukutana naye. Kauli hiyo inaashiria kuwa mkutano wa kihistoria unaopangwa kati yake na kiongozi huyo anayetengwa wa nchi ya bara Asia utaendelea. Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Trump ameandika kuwa alipokea ujumbe jana usiku kutoka kwa rais wa China Xi Jinping ukimweleza kuwa mkutano kati yake na Kim Jong Un uliendelea vizuri na kwamba Kim anatarajia kukutana naye. Ameendelea kusema kuwa kwa...
Mwanasiasa wa upinzani Kenya aliyeidhinisha kiapo cha kiongozi wa upinzani Raila Odinga kuwa ‘Rais wa Wananchi’ Januari Miguna Miguna ametimuliwa tena kutoka nchini humo. Mwanasiasa huyo ametimuliwa huku mzozo kuhusu uraia wake ukiendelea. Bw Miguna ameandika kwenye Facebook kwamba ameamka na kujipata yuko Dubai na kwamba anahitaji matibabu. Amesema anafahamu kwamba kuna mpango wa kumpeleka London lakini anataka kupanda ndege ya kurejea Nairobi pekee. Mwanasiasa huyo amesema amesindikizwa na afisa wa idara ya ujasusi. Serikali...