Mahakama ya rufaa nchini Brazil imeagiza kuwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Luiz Inacio Lula da Silva, ni sharti aanze kutumikia kifungo chake cha miaka kumi na miwili gerezani, baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika na ufisadi. Majaji sita kati ya kumi na mmoja wa mahakama ya rufaa walipinga rufaa hiyo huku watano kati yao wakimuunga mkono. Kesi hiyo imezua hali ya wasi wasi wa kisiasa nchini humo. Hatia hiyo imetokana na uchunguzi wa muda mrefu wa sakata...
Rufani ya Michael Richard Wambura bado kitendawili na hili ni baada ya kamati ya rufaa kuchelewa kutoa maamuzi. Je ni sahihi maamuzi kuchelewa ili haki itendeke au si sahihi kwa kuwa kamati hii imepokea taarifa ya pande zote mbili? Hebu tuzungumze hapa juu ya kile unachokiona kwenye sakata hili kwa kutoa comment yako....
Klabu ya soka ya Yanga ambayo Jumamosi hii inatarajiwa kucheza na Welayta Dicha ya Ethiopia katika kombe la shirikisho barani Afrika, itawakosa wachezaji wake wanne muhimu Wachezaji hao ambao wataukosa mchezo huo ni Kelvin Yondani, Obrey Chirwa, Papy Tshishimbi na Said Makapu. Wachezaji hao wataukosa mchezo huo kutokana na kuwa na kadi nyingi za njano ambazo walipata kwenye michuano ya kombe la klabu bingwa Afrika. Wapinzani hao wa Yanga wanatarajiwa kuwasili mchana wa leo (Jumatano) kwenye uwanja wa ndege wa...
Naibu Gavana wa jimbo la Ikweta kusini magharibu nchini Jamuhuri ya demokrasia ya Kongo ,Tathy Bikamba ameshtakiwa kwa tuhuma za ubakaji wa binti wa miaka 20 ambaye inadaiwa kuwa alimfanyia unyama huo baada ya kumpa dawa za kulevya. Gavana huyo anatarajiwa kufikishwa kinshasa kujibu tuhuma hizo mahakamani , ingawa wakili wake ametupia mbali tuhuma hizo. Taarifa kutoka duru za karibu za uchunguzi wa kesi hiyo ya kubaka vinasema kwamba gavana huyo alimbaka binti huyo siku ya Jumamosi. Bwana Bikamba ambaye...
Ni Cristiano Ronaldo tena anaendelea kuwanyamazisha wapinzani wa Real Madrid, dakika ya 3 tu alipiga shuti lake la 9 kwa Gianluigi Buffon na kufunga bao lake la 8 dhidi ya golikipa huyo, hili likiwa bao la kwanza katika mchezo huu. Dakika ya 64 Cristiano Ronaldo tena aliifungia Real Madrid bao la pili na kumfanya kuwa mchezaji katika historia aliyewafunga Juve mabao mengi (9) kabla ya Marcelo kufungia bao la 3 Real Madrid. Hii ni mara ya kwanza Juventus wanaruhusu kufungwa...
Klabu ya soka ya Manchester United hawana mpango kabisa ya kumuachia David de Gea kwenda Real Madrid. Man United inampango wa kumuongeze mkataba wa miaka mitano mchezaji huyo na kumlipa mshahara wa paundi 350,000 kwa wiki kabla ya kuanza kwa kombe la dunia, hiyo ni kwa mujibu wa gazeti la The Sun. De Gea ambaye alitua United mwaka 2011 akitokea Atletico Madrid, anatarajia kumaliza mkataba wake mwaka 2019. Golikipa huyo amekuwa tegemezi katika kikosi cha Man United huku katika msimu...
Wanamgambo wa kundi la kigaidi la al-Shabaab la nchini Somalia wamewauwa wanajeshi wanne wa Uganda katika shambulizi kubwa dhidi ya ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika, katika kambi iliyo Kusini mwa Mogadishu. Shambulizi hilo lilitokea jana Jumapili (Aprili 1) kwenye kambi iliyoko umbali wa kilomita 150 kusini mwa mji mkuu, Mogadishu. Awali, naibu gavana wa jimbo lilikotokea shambulizi hilo, Ali Noor Mohamed, hakubainisha idadi ya waliouawa, lakini alikiri kuwa wanajeshi kadhaa wa Uganda walipoteza maisha. Baadaye, msemaji wa...
Baada ya kuidhinishwa na Baraza la Serikali ya China, kamati ya Ushuru wa Forodha ya China imeamua kuwa itasimamisha upunguzaji wa ushuru wa Forodha kwa bidhaa 128 za aina 8 zinazoagizwa kutoka Marekani kuanzia jana tarehe 2 Aprili, huku ikiongeza ushuru wa Forodha kwa bidhaa hizo. Ikumbukwe kuwa tarehe 22 Machi, Rais Donald Trump wa Marekani amesaini kumbukumbu ya kuiwekea China vikwazo kwa mujibu wa matokeo ya ripoti kuhusu ukaguzi wa kipengele cha 301 cha sheria ya biashara, na kuagiza...
Simba itakuwa inakibarua dhidi ya wenyeji wa mji huo, Njombe Mji FC, katika mchezo wa ligi kuu bara utakaopigwa majira ya saa 10 jioni leo. Njombe Mji itakuwa inaikaribisha Simba ikiwa na kumbukumbu mbaya za kuondoshwa nje ya michuano ya Kombe la Shirikisho na Stand United ya mjini Shinyanga. Tayari timu zote mbili zimeshakamilisha maandalizi kuelekea mchezo mchezo huo wa...
– EFM imetimiza miaka 4 tangu kuanzishwa kwake. Nitumie nafasi hii kuishukuru Serikali kuu,TCRA kwakuendelea kutulea na kutuamini hadi sasa tumeongeza wigo wa Matangazo yetu. Niwashukuru MaKampuni na wadau ambao wameendelea kushirikiana nasi kwa namna moja au nyingine. Mwisho niwashukuru sana wasikilizaji na watendaji wote wa Efm. DODOMA,MORO,TABORA,KIGOMA na ARUSHA tunawafikia Mwezi huu.. HAPPY BIRTHDAY...