Matamshi ya mbunge wa Starehe nchini Kenya Charles ‘Jaguar’ Kanyi kuhusu kuwatishia raia wa kigeni wanaofanya kazi nchini Kenya yaliwasilishwa mbele ya kikao cha bunge ili kujadiliwa. Hatua hiyo inajiri huku Mbunge huyo akizuiliwa katika kituo cha polisi usiku kucha ambapo anasubiri kuwasilishwa mahakamani siku ya Alhamisi. Kulingana na mtandao wa runinga ya Citizen nchini Kenya, licha ya wabunge wengi kushutumu jinsi ambavyo bwana Jaguar alitoa hoja yake , baadhi yao walikubaliana kwamba kuna swala tata kuhusiana na raia wa...
Mvua kubwa imekuwa ikinyesha maeneo mengi Afrika Mashariki na kusababisha uharibifu wa mali na vifo. Nchini Kenya, watu zaidi ya 10 wamefariki baada ya kusombwa na maji ya mafuriko Wengi wao wamefariki wakisafiri kuelekea nyumbani au wakiwa kwenye magari wakijaribu kupitia maeneo yaliyofurika Je, unaweza kujikinga vipi hasa ukiwa safarini? Maafisa wa Mamlaka ya Taifa ya Usalama Barabarani (NTSA) pamoja na Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya wametoa ushauri ambao unaweza kukufaa sana wakati huu wa mvua. Fahamu kwamba wakati wa...
Mbeya. Viongozi wa Chadema wakiongozwa na mwenyekiti, Freeman Mbowe waliokwenda Gereza Kuu la Ruanda mkoani Mbeya kuwalaki Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga wamepigwa butwaa baada ya kuelezwa na askari magereza kwamba wameshatoka. Wakiwa nje ya gereza leo Mei 10, 2018, viongozi hao walifuatwa na askari na kuelezwa kwamba wawili hao wameshatoka. Magari mawili ya polisi yaliyokuwa yameimarisha ulinzi gerezani hapo nayo yaliondoka. Happiness Msonge, mkewe Sugu...
Mshambuliaji wa Paris St-Germain , 26, alifanya mazungumzo ya siri na Real Madrid mnamo mwezi Machi. Mchezaji huyo wa Brazil amedaiwa kutaka kuondoka mjiini Paris(AS, via Express). Mabingwa wapya wa ligi ya mabingwa Wolvehampton ambao wamepandishwa daraja katika ligi kuu ya Uingereza ni miongoni mwa wanaopigiwa upatu kumsaini mshambuliaji wa Everton Wayne Rooney, 32, mwisho wa msimu huu(Birmingham Mail) Lakini Rooney hatatoa uamuzi wa iwapo atasalia katika uwanja wa Goodison Park hadi pale hatma ya mkufunzi Sam Allardyce itakapoamuliwa(Star)....
Waziri mkuu wa zamani wa Malaysia Dr.Mahathir Mohamad amepata ushindi wa kihistoria katika uchaguzi mkuu uliofanyika katika hilo. Kiongozi huyo ameweza kukiangusha chama ambacho kimekuwa madarakani tangu mwaka 1957 ambacho kimekuwa kikidaiwa kujihusisha na nasuala ya rushwa na ufisadi. Dr.Mahathir ameshinda kwa idadi ya uwingi kura,na kukibwaga chama cha Barisan Nasional kilichotawala kwa zaidi ya miaka 60. Akiwa na umri wa miaka 92 Mhathir ameachana na kuitwa mstaafu na amerejea tena kuchukua nafasi ya mfuasi wake huyo wa zamani yaani...
Viongozi wa mataifa ya magharibi wanasema kuwa wataendelea kuuunga mkono makubaliano ya kinyuklia ya Iran muda mfupi baada ya Marekani kutangaza kuwa inajiondoa katika makubaliano hayo. Uingereza, Ufaransa na Ujerumani zinasema kuwa watafanya kazi pamoja na matiafa yote yaliosalia katika mkataba huo huku ikiitaka Marekani kutovuruga utekelezwaji wake. Mataifa mengine yalioweka mkataba huo wa 2015- Urusi na China pia yamesema yataendelea kuunga mkono makubaliano hayo. Iran imesema kuwa inafanya kazi kunusuru makubaliano hayo bila ya ushirikiano...
Mazungumzo ya muungano wa vyama nchini Italia yameshindikana,hivyo kuiacha nchi ikitakiwa kufanya uchaguzi mpya ama kuwa na serikali ya mpito hadi mwishoni mwa mwaka huu. Rais Sergio Mattarella amesema mazungumzo hayo ilikuwa ndiyo tegemeo la kulifikisha taifa hilo kwenye makubaliano kufuatia vyama vyote vilivyoshiriki uchaguzi mkuu mwezi machi kutofanikiwa kupata ushindi. Hakuna chama chochote binafsi kilichopata kura za kukiwezesha ushindi kama chama. Hata hivyo vyama viwili maarufu vya Five Star na The League,ndivyo vinavyochuana kwa...
Mji wa Nairobi umekumbwa na ukosefu mkubwa wa maji. Wakaazi wengi wa jiji hulazimika kununua maji kwa bei ghali kutoka kwa wachuuzi. Hali hii inaendelea licha ya mvua kubwa inayoendea kunyesha. Katika eneo la Rongai nje kidogo ya mji mkuu Nairobi, mmoja wa wakaazi wa eneo hili anaeleza jinsi imekuwa vigumu kapata maji. ”Nimeishi mtaa huu tangu miaka ya 80 na mpaka sasa, hatujawahi kuona tatizo kubwa la maji kama hili. Shida ya maji ni kubwa kiasi kwamba kutoka mwezi...
Mchezo wa pili wa El Clasico kati ya mahasimu Fc Barcelona na Real Madrid kwa msimu wa La Liga wa 2017/2018 uliopigwa katika dimba la Camp Nou ulimalizika kwa sare ya kufungana magoli 2-2. Mshambuliaji wa Barcelona Luis Suarez, ndio alianza kuipatia timu yake goli la kuongoza katika dakika ya kumi, ya mchezo, iliwachukua dakika nne kwa Madrid kusawazisha goli hilo kupitia kwa nyota wake Cristiano Ronaldo. katika dakika ya 52, mshambuliaji Lionel Messi, aliipatia klabu yake goli la pili...
Vladimir Putin anatarajiwa kuapishwa kwa muhula wa nne kama rais wa Urusi leo Jumatatu baada ya kushinda uchaguzi mnamo Machi. Amekuwa madarakani kwa miaka 18 kama rais na hata waziri mkuu, na wapinzani wameufananisha muda wake wa uongozi kama utawala wa mfalme. Polisi wa kupambana na fujo walikabiliana na waandamanaji wanaopinga utawala wake mjini Moscow na katika miji mingine Jumamosi. Kumekuwa na hofu kwamba huenda kutazuka ghasia tena leo Jumatau wakati anapoapishwa. Sherehe hiyo ya kuapishwa kwake itafanyika Kremlin mjini...