Barcelona yatoshana nguvu na Madrid El Clasico

Barcelona yatoshana nguvu na Madrid El Clasico

Like
544
0
Monday, 07 May 2018
Global News

Mchezo wa pili wa El Clasico kati ya mahasimu Fc Barcelona na Real Madrid kwa msimu wa La Liga wa 2017/2018 uliopigwa katika dimba la Camp Nou ulimalizika kwa sare ya kufungana magoli 2-2.
Mshambuliaji wa Barcelona Luis Suarez, ndio alianza kuipatia timu yake goli la kuongoza katika dakika ya kumi, ya mchezo, iliwachukua dakika nne kwa Madrid kusawazisha goli hilo kupitia kwa nyota wake Cristiano Ronaldo.
katika dakika ya 52, mshambuliaji Lionel Messi, aliipatia klabu yake goli la pili baada ya kuihada ngome ya ulinzi ya Real Madrid, Nyota toka Wales, Gareth Bale, alifunga goli la kusawazisha katika dakika ya 72 ya mchezo.

Barcelona walicheza pungufu ya mchezaji mmoja katika mchezo huo baada ya Sergi Roberto, kutolewa kwa kadi nyekundu, na klabu hiyo imendeleza rekodi yake nzuri ya kutopoteza mchezo hata mmoja katika msimu huu.

Lionel Messi anaongoza kwa ufungaji katika la Liga akiwa katupia kambani magoli 33 mpaka sasaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image caption
Lionel Messi anaongoza kwa ufungaji katika la Liga akiwa katupia kambani magoli 33 mpaka sasa
Mchezo wa pili wa El Clasico kati ya mahasimu Fc Barcelona na Real Madrid kwa msimu wa La Liga wa 2017/2018 uliopigwa katika dimba la Camp Nou ulimalizika kwa sare ya kufungana magoli 2-2.
Mshambuliaji wa Barcelona Luis Suarez, ndio alianza kuipatia timu yake goli la kuongoza katika dakika ya kumi, ya mchezo, iliwachukua dakika nne kwa Madrid kusawazisha goli hilo kupitia kwa nyota wake Cristiano Ronaldo.
katika dakika ya 52, mshambuliaji Lionel Messi, aliipatia klabu yake goli la pili baada ya kuihada ngome ya ulinzi ya Real Madrid, Nyota toka Wales, Gareth Bale, alifunga goli la kusawazisha katika dakika ya 72 ya mchezo.

Barcelona walicheza pungufu ya mchezaji mmoja katika mchezo huo baada ya Sergi Roberto, kutolewa kwa kadi nyekundu, na klabu hiyo imendeleza rekodi yake nzuri ya kutopoteza mchezo hata mmoja katika msimu huu.

Tayari Barcelona, ni mabingwa wa La Liga msimu huu wakiwa na alama 87, na wanasaliwa na michezo mitatu huku Madrid, wakiwa na alama 72 katika nafasi ya tatu na wakisaliwa na michezo miwili kabla ya ligi kumalizika.
Atletico Madrid walioko nafasi ya pili wakiwa na alama 75, wakicheza katika uwanja wao wa Wanda Metropolitano, walikubali kichapo cha magoli 2-0 Espanyol.
katika michezo mingine Las Palmas, walifungwa nyumbani na Getafe, kwa goli 1-0 na Alaves wakawatambia Malaga, kwa kuwachapa kwa magoli 3-0.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *