SASA SUGU HURU !

SASA SUGU HURU !

Like
518
0
Thursday, 10 May 2018
Local News

Mbeya. Viongozi wa Chadema wakiongozwa na mwenyekiti, Freeman Mbowe waliokwenda Gereza Kuu la Ruanda mkoani Mbeya kuwalaki Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga wamepigwa butwaa baada ya kuelezwa na askari magereza kwamba wameshatoka.
Wakiwa nje ya gereza leo Mei 10, 2018, viongozi hao walifuatwa na askari na kuelezwa kwamba wawili hao wameshatoka.
Magari mawili ya polisi yaliyokuwa yameimarisha ulinzi gerezani hapo nayo yaliondoka.
Happiness Msonge, mkewe Sugu akizungumza na MCL Digital amesema walipigiwa simu na kuelezwa kwamba wameshatoka na wako njiani wakielekea nyumbani.
Baadhi ya viongozi waliokuwepo ni mbunge wa Viti Maalumu, Sophia Mwakagenda, Meya wa Jiji la Mbeya, Mchungaji David Mwashilindi na madiwani.
Viongozi hao walianza kufika gerezani leo Mei 10, 2018 saa 12:45 asubuhi na kuingia ndani ya uzio wa gereza ambako askari waliwaondoa.
Sugu na Masonga walitiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha miezi mitano jela Februari 26 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya kwa kutoa lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli kwenye mkutano wa hadhara walioufanya Desemba 30 mwaka jana eneo la Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.
Wawili hao wameshatumikia adhabu hiyo kwa siku 73 ikiwa ni zaidi ya robo ya kifungo chao

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *