Tetesi za soka Ulaya Alhamisi 10.05.2018

Tetesi za soka Ulaya Alhamisi 10.05.2018

Like
377
0
Thursday, 10 May 2018
Sports

Mshambuliaji wa Paris St-Germain , 26, alifanya mazungumzo ya siri na Real Madrid mnamo mwezi Machi. Mchezaji huyo wa Brazil amedaiwa kutaka kuondoka mjiini Paris(AS, via Express).

Mabingwa wapya wa ligi ya mabingwa Wolvehampton ambao wamepandishwa daraja katika ligi kuu ya Uingereza ni miongoni mwa wanaopigiwa upatu kumsaini mshambuliaji wa Everton Wayne Rooney, 32, mwisho wa msimu huu(Birmingham Mail)

Lakini Rooney hatatoa uamuzi wa iwapo atasalia katika uwanja wa Goodison Park hadi pale hatma ya mkufunzi Sam Allardyce itakapoamuliwa(Star).

Klabu ya ligi ya Marekani ya DC United ina matumaini kwamba inaweza kumshawishi mfungaji huyo wa mabao mengi nchini Uingereza kujiunga nao(Washington Post)

Arsenal imempatia kiungo wa kati Jack Wilshere, 26, mkataba mpya wa miaka mitatu ikiwemo kuongeza mkataba huo kwa miezi 12 na hivyobasi kumzuia mchezaji huyo katika uwanja wa Emirates hadi 2022. (Mirror)

The Gunners wameanza mazungumzo ya kumsajili kipa wa Bayer Leverkusen Bernd Leno, 26, kuchukua mahala pake Petr Cech. (Bild, via Express)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *