Serikali ya muungano wa vyama yashindikana Italia

Serikali ya muungano wa vyama yashindikana Italia

Like
404
0
Tuesday, 08 May 2018
Global News

Mazungumzo ya muungano wa vyama nchini Italia yameshindikana,hivyo kuiacha nchi ikitakiwa kufanya uchaguzi mpya ama kuwa na serikali ya mpito hadi mwishoni mwa mwaka huu.
Rais Sergio Mattarella amesema mazungumzo hayo ilikuwa ndiyo tegemeo la kulifikisha taifa hilo kwenye makubaliano kufuatia vyama vyote vilivyoshiriki uchaguzi mkuu mwezi machi kutofanikiwa kupata ushindi. Hakuna chama chochote binafsi kilichopata kura za kukiwezesha ushindi kama chama.
Hata hivyo vyama viwili maarufu vya Five Star na The League,ndivyo vinavyochuana kwa karibu.
Mazungumzo hayo yaliyoshindikana yalikuwa na lengo kuunda serikali ya muungano,japo kuwa chama kikuu cha kilipinga hatua hiyo ya ama kuungana na chama chama cha mrengo wa kulia ama ule wa kushoto.

Akizungumza siku ya jumatatu kwa njia ya televisheni rais Mattarella alitoa rai kwa viongozi wa vyama kunga mkono serikali huru isiyoegemea upande wowote na hasa baada ya kushindikana kuundwa kwa serikali ya muungano wa vyama na kusisitiza kwamba hawawawezi kuendelea kusubiria bila ya kuwa na serikali.

Mattarella ameongeza kuwa serikali hiyo hiyo isiyofungamana na upande wowote wa vyama,ndiyo iwe na jukumu la kuandaa bajeti yam waka 2019 ili kuliepusha taifa hilo kushuka kiuchumi.
Serikali hiyo ya mpito itaendesha taifa hilo hadi mwishoni mwa mwaka,na kisha baadaye kufikia ukomo baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2019.
Hadi sasa si chama cha Five Star movement ama The League ambacho kimeonyesha uungaji mkono mawazo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *