Marekani yajiondoa katika mpango wa nyuklia wa Iran

Marekani yajiondoa katika mpango wa nyuklia wa Iran

Like
406
0
Wednesday, 09 May 2018
Global News

Viongozi wa mataifa ya magharibi wanasema kuwa wataendelea kuuunga mkono makubaliano ya kinyuklia ya Iran muda mfupi baada ya Marekani kutangaza kuwa inajiondoa katika makubaliano hayo.
Uingereza, Ufaransa na Ujerumani zinasema kuwa watafanya kazi pamoja na matiafa yote yaliosalia katika mkataba huo huku ikiitaka Marekani kutovuruga utekelezwaji wake.
Mataifa mengine yalioweka mkataba huo wa 2015- Urusi na China pia yamesema yataendelea kuunga mkono makubaliano hayo.

Iran imesema kuwa inafanya kazi kunusuru makubaliano hayo bila ya ushirikiano wa Marekani.
”Mataifa yetu yataendelea kuunga mkono makubaliano hayo na yatafanya kazi na mataifa yanaoendelea kuunga mkono mkataba huo”, Uingereza, Ujerumani na Ufaransa zilisema katika taarifa ya pamoja.
Siku ya Jumanne rais wa Iran Hassan Rouhani alisema: “Nimeagiza wizara ya maswala ya kigeni kujadiliana na mataifa ya Ulaya ,China na Urusi katika majuma yajayo”.
”Iwapo tutaafikia malengo ya makubaliano haya kwa ushirikikiano wa wanachama wengine basi makubaliano hayo yataendelea kuheshimiwa”.
Mkakati wa pamoja uliizuia Iran kuendelea na mpango wake wa kinyuklia huku Umoja wa mataifa ukikubali kuiondolea vikwazo Iran vilivyowekwa pamoja na, Marekani na bara Ulaya.

Katika taarifa katika runinga ya taifa siku ya Jumanne , rais alisema kuwa Marekani itajiondoa katika mkakati huo wa pamoja JCPOA.
Aliutaja kuwa mkataba mbaya unaopendelea upande mmoja ambao haungewahi kuafikiwa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *