Yanga kuwakosa wachezaji wanne kikosi cha kwanza kombe la shirikisho

Yanga kuwakosa wachezaji wanne kikosi cha kwanza kombe la shirikisho

Like
618
0
Wednesday, 04 April 2018
Local News

Klabu ya soka ya Yanga ambayo Jumamosi hii inatarajiwa kucheza na Welayta Dicha ya Ethiopia katika kombe la shirikisho barani Afrika, itawakosa wachezaji wake wanne muhimu

Wachezaji hao ambao wataukosa mchezo huo ni Kelvin Yondani, Obrey Chirwa, Papy Tshishimbi na Said Makapu.

Wachezaji hao wataukosa mchezo huo kutokana na kuwa na kadi nyingi za njano ambazo walipata kwenye michuano ya kombe la klabu bingwa Afrika.

Wapinzani hao wa Yanga wanatarajiwa kuwasili mchana wa leo (Jumatano) kwenye uwanja wa ndege wa Mwl. JK Nyerere jijini Dar es Salaam.

 

Comments are closed.