Gavana atuhumiwa kwa ubakaji DRC

Gavana atuhumiwa kwa ubakaji DRC

Like
324
0
Wednesday, 04 April 2018
Slider

Naibu Gavana wa jimbo la Ikweta kusini magharibu nchini Jamuhuri ya demokrasia ya Kongo ,Tathy Bikamba ameshtakiwa kwa tuhuma za ubakaji wa binti wa miaka 20 ambaye inadaiwa kuwa alimfanyia unyama huo baada ya kumpa dawa za kulevya.

Gavana huyo anatarajiwa kufikishwa kinshasa kujibu tuhuma hizo mahakamani , ingawa wakili wake ametupia mbali tuhuma hizo.
Taarifa kutoka duru za karibu za uchunguzi wa kesi hiyo ya kubaka vinasema kwamba gavana huyo alimbaka binti huyo siku ya Jumamosi.
Bwana Bikamba ambaye kwa sasa yuko gerezani anatarajiwa kufikishwa mahakamani hii leo ili aweze kujibu mashtaka yake ya kumwekea dawa ya kulevywa na kumfanyia tendo la ngono binti bila idhaa yake.
Wakili wa gavana huyo, Imbambo Engulu ametupilia mbali tuhuma hizo na kushutumu mahakama ya jimbo hilo kwa kumzuia gavana huyo bila kujali na cheo chake
“Kushikwa kwake ni kama uonevu, tuliomba wamuzuie kwanza nyumba kwake badala ya kumuweka gerezani moja kwa moja, majaji hawakukubali ombi letu, Nawambia kweli kuwa gavana hakufanya kitendo hicho, ni uongo.”
Waziri wa sheria ,Faida mwangiliwa ambaye pia ni miongoni mwa wanaharati wa haki za wanawake ameomba sheria kumhukumu vikali gavana huyo ikiwa tuhuma hizo zitathbitishwa na mahakama

Kesi za ubakaji zimeripotiwa nyingi nchini jamuhuri ya kidemokrasi ya kongo, idadi kubwa ya kesi imefanywa na waasi na wanajeshi wa taifa husuan mashariki mwa DRC.
Katika miaka ya hivi karibuni, serikali ya kongo tayari kuathibu vikali askari kadhaa na maafisa wa jeshi la Kongo wengi kwa kuwapa kifungo cha maisha .

Comments are closed.