RONALDO REKODI MPYA UGENINI

RONALDO REKODI MPYA UGENINI

Like
856
0
Wednesday, 04 April 2018
Sports

Ni Cristiano Ronaldo tena anaendelea kuwanyamazisha wapinzani wa Real Madrid, dakika ya 3 tu alipiga shuti lake la 9 kwa Gianluigi Buffon na kufunga bao lake la 8 dhidi ya golikipa huyo, hili likiwa bao la kwanza katika mchezo huu.

Dakika ya 64 Cristiano Ronaldo tena aliifungia Real Madrid bao la pili na kumfanya kuwa mchezaji katika historia aliyewafunga Juve mabao mengi (9) kabla ya Marcelo kufungia bao la 3 Real Madrid.

Hii ni mara ya kwanza Juventus wanaruhusu kufungwa mabao 3 nyumbani tangu mwaka 2009 walipofungwa bao 4-1 na Bayern Munich, Juventus walimaliza wakiwa pungufu baada ya Paulo Dyabala kuoneshwa kadi nyekundu.

Kama hujui tu ni kwamba bao la kwanza la Madrid ndio bao la mapema zaidi kwa Cristiano Ronaldo kuwahi kufunga katika Champions League, huku sasa Mreno huyo akiwa na mabao 38 katika msimu huu(michuano yote) ikiwa ni idadi kubwa kuliko mchezaji yeyote barani Ulaya.

Tangu klabu ya Juventus wahamie katika uwanja wao mpya mwaka 2011 hawajawahi kupokea kipigo kama hiki katika uwanja huo katika mashindano yoyote yale.

 

Comments are closed.