Teknolojia ya video (VAR) imeibeba timu ya taifa ya Itali kufanikiwa kuchomoza na sare ya bao 1 – 1 dhidi ya Uingereza mchezo wa kirafiki. Wakati Uingereza ikifanikiwa kuongoza mchezo huo baada ya kupata bao lake dakika ya 26 kupitia kwa Jamie Vardy kunako dakika ya 87 mchezaji wa Itali, Lorenzo Insigne akaisawazishia timu hiyo kwa msaada wa teknolojia ya VAR huko Wembley. Timu ya taifa ya Uingereza ilikuwa ikitarajia kupata ushindi wake wa pili baada ya kuifunga Netherlands kwa...
Taifa Stars imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika mchezo wa kirafiki uliopigwa jana. Stars ilifunga mabao yake kipindi cha pili baada ya kile cha kwanza kwenda suluhu ya 0-0 kupitia kwa Mbwana Samatta na Shiza Ramadhan Kichuya. Stars ilipata ushindi huo ikiwa imetoka kupoteza mchezo uliopita dhidi ya Algeria kwa jumla ya mabao 4-1 huko Algiers. Kocha wa Taifa Stars, Mayanga ameeleza kuwa mchezo huo ulikuwa vizuri kutokana na vijana wake kuonesha...
Baada ya siku ya uvumi wa siku nyingi, imethibitishwa kwamba kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amezuru China. Ziara hiyo, ambayo ilithibitishwa na China na Korea Kaskazini, ndiyo ya kwanza inayofahamika ya Bw Kim nje ya taifa lake tangu alipochukua mamlaka mwaka 2011. Bw Kim alifanya “mazungumzo ya kufana” na kiongozi wa China Xi Jinping mjini Beijing, shirika la habari la China, Xinhua liliripoti. China ni mshirika mkuu wa Korea Kaskazini kiuchumi na baadhi ya wachambuzi wanasema uwezekano wa wawili...
Kifusi kutoka kwa kituo cha maabara cha safari za anga cha China, kinaweza kupasuka na kuanguka duniani Ijumaa,wanasayansi wanaokifanyia uchunguzi wanasema. Kituo hicho cha Tiangong-1 ni sehemu ya mpango wa safari za anga za mbali wa Uchina, na wa sampuli ya kituo cha safari za anga za mbali cha binadamu wa mwaka 2022. Kiliwekwa kwenye uzio mwaka 2011 na miaka mitano baadae kikamilisha shughuli yake, na baadae kilitarajiwa kuanguka duniani. Muda na mahala kitakapoangukia ni vigumu kutabiri kwasababu sasa hakidhibitiwi....
Uvumi waenea kuhusu ziara ya Kim Jong-un Beijing Uvumi kuhusu ziara ya kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un mjini Beijing umehanikiza katika wakati ambapo kukiwa na gumzo kuhusu maandalizi ya mkutano wa kilele kati ya kiongozi huyo wa Korea Kaskazini na rais Trump. Mji Mkuu wa China Beijing, ulikuwa chini ya usalama mkali Jumanne, huku kukiwa na uvumi kwamba kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un alikuwa anafanya ziara ya kustukiza, kufuatia ripoti za kuwasili kutoka Pyongyang, kwa treni maalumu iliyopokelewa...
Wakili wa upinzani aliyeidhinisha kiapo cha Bw Raila Odinga alipokuwa anajiapisha kuwa ‘Rais wa Wananchi’ mwezi Januari bado amekwama katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta, Nairobi. Bw Miguna Miguna alijaribu kurejea Kenya Jumatatu lakini akazuiwa kuingia baada yake kudaiwa kutowasilisha pasipoti ya Canada ambayo ilitumiwa kumsafirisha kwa nguvu hadi Canada. Wakili huyo alisisitiza kwamba ni raia wa Kenya na hafai kuzuiwa kurejea. Taarifa zinasema Bw Miguna, ambaye pasipoti yake ya Kenya ilitwaliwa na polisi kabla ya kuondolewa...
Michael Petter ambae ni mshiriki na mshindi wa #ShikaNdinga2017 akitoa mrejesho wa maisha yake ya biashara baada ya...
Katika kusherekea Miaka minne ya uwepo wa E Fm radio tunayo furaha sana na tuna kila sababu za kusherekea uwepo wetu. Wakati tunaanza tulikuwa na wafanyakazi 10 tu lakini leo hii E-fm imeajiri wafanyakazi zaidi ya 100 moja, wakati tunaanza tulikuwa tunasikika Dar-es-alaam pekee lakini leo hii E-fm inasikika kwenye mikoa 6 pia tumeweza kuwawezesha wadau wetu na mdau wetu mkubwa ni msikilizaji wa E-fm tukiwa na bidhaa kama SHIKA NDINGA ambapo tumefanikiwa kutoa magari ya biashara pamoja pikipiki...
Australia imekuwa nchi ya karibuni kufukuza wanadiplomasia wa Urusi kutoka nchini kwake kutokana na shambulio la jasusi wa zamani wa urusi nchini Uingereza Sergei Skripal na binti yake ambao wako katika hali mbaya kiafya. Novichok: Sumu iliyotumiwa kumshambulia jasusi wa Urusi Waziri mkuu Malcolm Turnbull amesema uamuzi huo unatokana na shambulio hatari la kutumia kemikali za neva zinazotengezwa na Urusi na zilitomiwa mara mwisho vita vya pili vya dunia.Idadi ya wanadiplomasia wa Urusi wanaofukuzwa inazidi kuongezeka, na hii ndio idadi...