Sports

ODEGAARD ATUA BERNABEU
Slider

  Real Madrid imefikia makubaliano ya kumsajili mshambuliaji kutoka klabu ya Stromsgodset ya Norway Martin Odegaard mwenye umri wa miaka 16. Real Madrid hawakuweka wazi makubaliano yao na mshambuliaji huyo lakini vyombo vya habari vya Hispania vimeripoti kuwa wamelipia si chini ya euro milioni tatu kumpata mchezaji huyo Anatarajiwa kuungana na klabu ya Real Madrid timu B ambayo inaongozwa na mwalimu Zinedine...

Like
230
0
Thursday, 22 January 2015
MPINZANI WA MAYWEATHER ATANGAZA KUACHA MUZIKI
Entertanment

Hii ndio kauli ya bingwa wa masumbwi duniani kutokea nchini Ufilipino Manny Pacquiao kwenye vyombo vya habari Pacquiao ametangaza rasmi kuachana kabisa na shughuri za kimuziki na kusema kwamba anaupenda muziki ila hadhani kama muziki unampenda “I love music, but I don’t think music loves me.” Pacquiao amesema hatotoa albam mpya tena . Pacquiao kwa sasa anapromote documentary lakini hadi hivi sasa amesema anajivunia mafanikio aliyoyapata kupitia muziki, aidha Pacquiao ameongeza ya kuwa albam yake ya kwanza ilifikia mauzo ya...

Like
261
0
Thursday, 22 January 2015
TETESI ZA MAGAZETI YA NG’AMBO
Slider

TETESI ZA MAGAZETI: Klabu ya Manchester United ipotayari kuvunja rekodi ya usajili kwa kuweka mezani kitita cha paundi milioni 112 ili kumsajili beki wa kati wa klabu ya PSG MARQUINHOS. (Daily Mirror) Klabu ya Everton ipotayari kumpiga bei mshambuliaji wao KEVIN MIRALLAS katika dirisha hili la usajili. (Metro)  Klabu ya Chealsea ipotayari kumsajili mshambuliaji wa klabu ya Fiorentina JUAN CUADRADO endapo watafanikiwa kuwauza wakina MOHAMED SALAH  na ANDRE SCHURRLE. (Daily Mirror)  Kiungo wa klabu ya Manchester City JAMES MILNER amesema...

Like
244
0
Wednesday, 21 January 2015
CRISTIANO RONALDO AMWAGANA NA SHAYK
Slider

Mchezaji bora wa dunia Cristiano Ronaldo na mwanamitindo wa Urusi Irina Shayk wameripotiwa kuachana baada ya miaka mitano ya mahusiano yao. Tetesi hizo zilianza kusambaa mara baada ya Shyk kukosa kuhudhuria kwenye sherehe za kutoa tuzo za mchezaji bora duniani wiki iliyopita na utata ulikuja zaidi pale muwakilishi wa mwanamitindo Shayk kuzungumza na waandishi wa habari huko marekani na kuweka wazi kuwa wawili hao hawapo pamoja tena Mwanamitindo huyo mwenye umri wa miaka 29 alijizolea umaarufu zaidi duniani baada ya...

Like
214
0
Wednesday, 21 January 2015
KATANGA ATEULIWA KUWA AFISA HABARI WA DRFA
Slider

Chama cha soka mkoa wa Dar es salaam DRFA jana kilimtangaza Mwandishi na mtangazaji wa Habari za michezo kutoka kwenye kituo hiki cha EFM kwenye dawati la michezo la E sport Omary Katanga kuwa msemaji Mpya wa chama hicho. Katanga anachukuwa nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Mohamed Mharizo ambae amekubaliana na uongozi kuachia nafasi hiyo. Katanga maarufu kama mlinda mlango namba moja ulimwenguni anawika katika medali ya utangazaji wa habari za kimichezo katika kipindi cha Esport,kinachoruka kila siku sa moja hadi saa...

Like
331
0
Wednesday, 21 January 2015
TETESI ZA MAGAZETI YA NG’AMBO
Slider

  Beki wa kati wa klabu ya Borussia Dortimund MATS HUMMEL amesema kuwa hana mpango wa kuihama klabu hiyo kwa sasa. (Daily Express)  Klabu ya Manchester United imeandaa paundi milioni 15 ili kumsajili beki wa klabu ya Barcelona GERARD PIQUE (Telegraph) Klabu ya Wolfsburg ipotayari kutoa kitita cha paundi milioni 23 ili kumsajili mshambuliaji wa klabu ya Chealsea ANDRE SCHURRLE lakini klabu hiyo imekataa dau hilo inahitaji paundi milioni 30. (Daily Star)    Kiungo wa klabu ya Arsenal FRANCIS COQUELIN...

Like
280
0
Tuesday, 20 January 2015
AFCON: MAKALA MAALUM YA UCHAMBUZI WA SOKA TAIFA LA AFRIKA KUSINI
Slider

Ikiwa michuano ya Afcon tayari imeanza kwenye hatua za makundi huko EQUTORIAL GUINEA   macho yetu leo hii yanalitazama taifa la Afrika kusini, Afrika kusini ni nchi inayopatikana kusini mwa bara la Afrika ikiwa karibu na bahari ya Atlantic na bahari ya Hindi,nchi hiyo imepakana na Zimbabwe,Botswana,Namibia,Lesotho na Swaziland.Taifa hilo limepata uhuru kutoka kwa wadachi mwaka 1994 Afrika kusini ni nchi ya pili inayoongoza kiuchumi barani Afrika na inashika nafasi ya 34 kiuchumi duniani, Taifa la Afrika Kusini linamchanganyiko wa watu...

Like
269
0
Tuesday, 20 January 2015
AFCON: MOUSSA SOW AIINUA SENEGAL
Slider

Mshambuliaji wa Senegal Moussa Sow jana aliinua timu yake baada ya kufunga bao la muda wa lala salama hivyo kuifanya Senegal kuibuka na ushindi dhidi ya Black stars ya Ghana   Bao hilo lilipatikana mnamo dakika ya 90 na kuipa Senegal alama zote tatu Mchezaji wa Ghana Andrew Ayew alifunga mkwaju wa Penalti baada ya kiungo wa kati wa Everton Christian Atsu kuangushwa katika eneo la hatari. Lakini Senegal ilijitahidi na kupiga chuma cha goli la Ghana kupitia mchezaji Kara...

Like
338
0
Tuesday, 20 January 2015
MATOKEO YA LIGI KUU TANZANIA BARA
Slider

Polisi Moro imeibana Coastal Union kwao Mkwakwani mjini Tanga. Wageni hao wameikomalia Coastal na kuilazimisha sare ya bila kufungana. Polisi Moro ilipoteza nafasi mbili za kufunga katika kipindi cha kwanza. Lakini Coastal nayo ilishindwa kufunga katika kipindi cha pili baada ya kupata nafasi zaidi ya mbili. Hata hivyo, Polisi ilionyesha soka safi la pasi za uhakika na kumiliki mpira muda mwingi licha ya kuwa ugenin MECHI YA COASTAL UNION DHIDI YA YANGA YAAHIRISHWA Mechi kati ya Coastal Union dhidi Yanga...

Like
320
0
Monday, 19 January 2015
AFCON: BAADA YA MBABE KUKOSEKANA KUNDI B LEO TIMU ZA KUNDI C ZITASHUKA DIMBANI
Slider

Mataifa yanayounda kundi B ambayo ni Drc, Tunisia, Cape verde na Zambia katika michuano ya kombe la mtaifa Afrika zimejikuta zikikosa mbabe baada timu zote kuibuka na sare ya kufungana 1-1  Mchezo wa kwanza wa kundi hilo ulipigwa kwakuikutanisha Zambia na Congo ambapo Zambia ilitangulia kuziona nyavu za Drc kupitia mnamo dakika ya pili bao lililofungwa na mchezaji wake Given Singuluma na kudumu hadi mapumziko Bao hilo lilisawazishwa na mchezaji wa Drc Yannick Bolasie kwenye dakika ya 66 hadi mwisho...

Like
249
0
Monday, 19 January 2015
MAKALA MAALUM YA UCHAMBUZI WA SOKA TAIFA LA DRC
Slider

Katika harakati za maandalizi ya vikosi vya timu za mataifa 16 kutoka katika bara la afrika kuelekea kunako michuano mikubwa yakusaka taifa bingwa katika mchezo wa soka inayo taraji kuanza mnamo tarehe 17/01/2015. Leo hii macho na masikio ya mashabiki walio wengi yanataka kusikia ama kuona ni taifa gani litaibuka kidedea katika michuano hiyo? Tutazame ubora na mafanikio ya timu mojamoja ambapo kwa sasa machoyetu yanaitazama timu ya taifa ya CONGO DRC ikiwa katika kundi “B” likiongozwa na Zambia,Tunisia na...

Like
421
0
Monday, 19 January 2015