IDADI YA WAGONJWA WA KIPINDUPINDU YAPUNGUA DAR

IDADI YA WAGONJWA WA KIPINDUPINDU YAPUNGUA DAR

Like
292
0
Wednesday, 25 November 2015
Local News

IDADI ya wagonjwa wa kipindupindu jijini Dar es salaam imeelezwa kupungua  kufikia wagonjwa kumi na mbili kwa mkoa mzima, huku wilaya ya Temeke pekee ikiwa na wagonjwa saba, Kinondoni wagonjwa wanne na Ilala ikiwa na mgonjwa mmoja

 

Mratibu wa Magonjwa  ya kuambukiza wa Jiji la Dar es salaam  Bw. Alex Mkamba ameyasema hayo ofisini kwake ambapo ameeleza pia ni  jinsi gani mkoa umefanikisha kupambana na kipindupindu kwa kuzingatia usafi katika jiji.

 

Mpaka sasa jumla ya watu 55 wamefariki dunia kwa ugonjwa wa kipindupindu jijini Dar es salaam

Comments are closed.