MAREKANI: IDADI YA WATU WANAOJIUA YAONGEZEKA

MAREKANI: IDADI YA WATU WANAOJIUA YAONGEZEKA

Like
286
0
Friday, 22 April 2016
Global News

TAKWIMU rasmi za serikali zinaonesha idadi ya watu wanaojiua nchini Marekani imeongezeka kwa kiasi kikubwa.

Takwimu hizo kutoka Kituo cha Taifa cha Takwimu za Afya zinaonyesha kuwa viwango vya watu kujiua vimeongezeka kwa karibu asilimia 25 katika kipindi cha miaka 15 iliyopita.

Utafiti huo uliofanyika kwa jinsia zote umeonesha kwamba viwango vya wanawake kujiua ndivyo vilivyoongezeka zaidi, vikipanda kwa asilimia 36 vikiwahusisha zaidi wanawake wa umri wa makamo.

                                                

Comments are closed.