MAREKANI: MAUAJI YA SOKWE YAZUA HISIA

MAREKANI: MAUAJI YA SOKWE YAZUA HISIA

Like
293
0
Monday, 30 May 2016
Local News

Mauaji ya Sokwe katika mbuga ya wanyama ya Cincinnati nchini Marekani yamezua utata katika mtandao wa Twitter.

Sokwe huyo anadaiwa kumuangusha na kumvuruta kijana wa miaka minne.

Sokwe huyo alipigwa risasi na kuuawa kufuatia kisa hicho cha kumvuruta mtoto.

Watu katika mtandao wamesema sokwe huyo kwa jina Harambe hangestahili kuuawa kwani hakuwa na niya ya kumdhuru mtoto huyo.

Wengi walitumia#hakikwaHarambe.

Huku wengine wakisema wazazi wa kijana huyo ndio wa kulaumiwa kwa kukosa kumuangalia mwanawe.

Maafisa wa shirika la wanyama pori walisema walichukua hatua hiyo dhidi ya sokwe huyo baada ya maisha ya mtoto huyo kuwa hatarini.

Zaidi ya watu elfu 60 wametia saini malalamiko hayo ya kipekee wakitaka wazazi wa kijana huyo kuchuliwa hatua ya kukosa kumlinda mwanawe na uzembe uliosababisha kifo cha

Comments are closed.