WAKIMBIZI ZAIDI KUREJESHWA UTURUKI LEO

WAKIMBIZI ZAIDI KUREJESHWA UTURUKI LEO

Like
209
0
Friday, 08 April 2016
Global News

KUNDI la pili la wahamiaji wanatarajiwa kurejeshwa nchini Uturuki kutoka Ugiriki baadaye hii leo, kama sehemu ya mkataba ulioafikiwa na Muungano wa Ulaya, wa kupunguza idadi wa wakimbizi wanaofika Ulaya.

 

Kundi la kwanza liliwasili Uturuki, siku ya Jumatatu, lakini tangu wakati huo mpango huo umekwama kwa sasa ambapo idadi kubwa ya wahamiaji wanaomba hifadhi nchini Ugiriki.

 

Inaaminika kuwa boti zingine mbili zitawasili leo, Ijumaa, ikiwa na wahamiaji waliofukuzwa kutoka Ugiriki chini ya mkataba huo wa EU.

Comments are closed.