AMIR KHAN KUPAMBANA NA ALVAREZ

AMIR KHAN KUPAMBANA NA ALVAREZ

Like
230
0
Wednesday, 03 February 2016
Slider

Bondia mwingereza Amir khan anatarajia kupigana na bondia kutoka Mexico sauli Alvarez kuwania mkanda wa WBC katika uzito wa kati mnamo mei saba mjini Las Vegas.

Khan mwenye miaka 29, ambaye ni bingwa wa dunia katika uzito wa welter hajapigana tangu apigwe na Chris Algieri mjini New York mwezi Mei.

Kwa upande wake Alvarez mwenye miaka 25, amewahi kumpiga bondia Miguel Cotto kwa pointi mjini Las Vegas mwezi Novemba.

Mpaka sasa amepoteza pambano mara moja huku akishinda mara 46 katika mapambano yake.

Comments are closed.