ASKOFU MATHIAS JOSEPH AFARIKI DUNIA

ASKOFU MATHIAS JOSEPH AFARIKI DUNIA

Like
415
0
Wednesday, 13 April 2016
Local News

 

ASKOFU msitaafu wa Jimbo Katoliki la Dodoma, Mhashamu Askofu Mathias Joseph Issuja, amefariki dunia.

 

Askofu isuja ambaye alizaliwa mwaka 1929 alipata daraja hilo Takatifu mwaka 1972 ambapo aliwekwa wakfu na Hayati Kardinali Laurean Rugambwa na kustaafu mwaka 2005 akiwa Askofu wa Jimbo la Dodoma.

 

Efm imezungumza kwa njia ya simu na Katibu mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania-TEC, Padri Raymond saba ambaye amesema kuwa Askofu mstaafu Issuja, amefariki usiku wa kuamkia leo huko katika Hospitali ya Mtakatifu Gaspar Itigi alikokuwa akipatiwa matibabu lakini pia ametaja sababu ya kifo hicho pia ni uzee.

Comments are closed.