BARAZA LA USALAMA LA UN KUFANYA MIKUTANO YA DHARURA LEO

BARAZA LA USALAMA LA UN KUFANYA MIKUTANO YA DHARURA LEO

Like
225
0
Monday, 26 January 2015
Global News

BARAZA la usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kufanya mikutano ya dharura hii leo kuijadili mizozo ya Ukraine na Yemen.

Lithuania imesema iliwasilisha ombi kufanyike mkutano wa wazi kuhusu mzozo wa Ukraine.

Baraza hilo la usalama limekutana takriban mara 30 kuujadili mzozo wa Ukraine tangu uanze lakini limeshindwa kuchukua hatua madhubuti kutokana na wanachama wa kudumu kama Urusi kutumia kura ya turufu kupinga maamuzi.

 

Comments are closed.