BARCLAYS PRIMIER LEAGUE: CHELSEA KUMENYANA NA STOKE CITY LEO

BARCLAYS PRIMIER LEAGUE: CHELSEA KUMENYANA NA STOKE CITY LEO

Like
319
0
Monday, 22 December 2014
Slider

Vinara wa Ligi kuu nchini England, klabu ya Chelsea leo wanashuka tena dimbani kumenyana na klabu ya Stoke City katika uwanja wa Brittania majira ya saa tano kamili usiku kwa saa za Afrika ya Mashariki.

Chelsea inayonolewa na kocha Jose Mourinho inaongoza ligi hiyo ikiwa na alama 39 sawa na klabu ya Manchester City iliyopata ushindi mnono wiki iliyopita dhidi ya Crystal Palace.

Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amemuomba refarii wa mchezo huo wa leo, Swarbrick awe makini katika maamuzi yake kwani klabu ya Stoke City inasifika kwa kutumia nguvu sana dhidi ya wapinzani wao.

Stoke City inashika nafasi ya 13 katika msimamo wa ligi kuu nchini England ikiwa imeshinda michezo mitano, ikitoka sare mara nne huku wakipoteza michezo saba na kujikusanyia jumla ya alama kumi na tisa.

Comments are closed.