BARTOMEU AMMWAGIA SIFA MESSI

BARTOMEU AMMWAGIA SIFA MESSI

Like
208
0
Monday, 24 November 2014
Slider

Rais wa klabu ya FC Barcelona amemmwagia sifa nahodha wa timu ya taifa ya Argentina na mshambuliaji wa klabu hiyo, Lionel Messi kuwa ndio mchezaji bora kabisa kuwahi kutokea.

Josep Maria Bartomeu ambaye ni rais wa klabu ya Barcelona inayonolewa na kocha Luis Enrique amezungumza hayo baada ya kushuhudia Messi akivunja rekodi ya magoli ndani ya La Liga iliyokuwa ikishikiliwa na marehemu Telmo Zarra.

Messi mwenye umri wa miaka ishirini na saba amefikisha jumla ya magoli mia mbili na hamsini na tatu na kuvunja rekodi ya Zarra ya magoli mia mbili hamsini iliyodumu kwa zaidi ya miaka hamsini.

Mshambuliaji huyo pia anashikilia rekodi ya magoli katika klabu bingwa Ulaya akiwa sawa na mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Real Madrid, Raul Gonzalez wakiwa na magoli sabini na moja.

Comments are closed.