BMW LAMTOKEA PUANI JORDIN SPARKS

BMW LAMTOKEA PUANI JORDIN SPARKS

Like
263
0
Saturday, 17 January 2015
Entertanment

Kama uliwahi kufiria kupewa zawadi ya gari na mpenzi wako kikubwa kwa sasa ni kujiuliza mara mbili kwamba iwapo mkiachana hali itakuwaje?.

Baada ya kuachana kwa njia salama na amani Jason Derulo na Jordin Sparks miezi kadhaa nyuma huku kila mmoja wao akiyazungumzia mahusiano yao kama ni mambo binafsi hivyo hawakuwa na sababu ya kuweka wazi.

Sasa Jordin Sparks alipokuwa akihijiwa kwenye moja ya vipindi vya redio kuhusu mahusiano yao ndipo alipogusia gari aina ya BMW alilopewa na aliekuwa mpenzi wake Jason Derulo kuwa halikununuliwa bali ni la kukodi

Katika kujibu tuhuma hizo Jason kupitia ukurasa wake wa instagram na kuanika maneno haya ‘Women Lie, Men Lie, Numbers Don’t Lie! #WhyLease #BreakfastClub @cthagod @djenvy @angelayee@jordinsparks

Akimaanisha sote wanaume na wanawake tunadanganya lakini namba hazidanganyi huku akihoji kwanini iwe ya kukodi, akiambatanisha stakabadhi ya malipo ya gari hilo akiwa amewatag watangazaji wa kipindi maarufu Marekani ya Breakfast club

Comments are closed.