CHADEMA YAMVUA RASMI UANACHAMA ZITTO KABWE

CHADEMA YAMVUA RASMI UANACHAMA ZITTO KABWE

Like
281
0
Tuesday, 10 March 2015
Local News

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Leo kimemvua Rasmi Uanachama aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mheshimiwa ZITTO KABWE kwa madai ya kushindwa kutekeleza Masharti ya Katiba ya chama hicho.   Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es salaam Mwanasheria Mkuu wa chama hicho Mheshimiwa TUNDU LISU amesema kuwa, mnamo mwaka jana Mheshimiwa ZITTO alifungua Mashitaka katika Mahakama Kuu akizuia vyombo vya Chama kukaa kujadili na kufanya maamuzi yanayohusu yeye kuendelea kuwa Mwanachama wa Chama hicho.

Amesema kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja vyombo vya chama vilizuiliwa na Mahakama kukaa kujadili  na kuzungumzia au kutoa maamuzi kuhusiana na masuala yanayomuhusu Mheshimiwa ZITTO

Comments are closed.