CHAGUZI SERIKALI ZA MITAA ZANGIA DOSARI

CHAGUZI SERIKALI ZA MITAA ZANGIA DOSARI

Like
257
0
Monday, 15 December 2014
Local News

UCHAGUZI wa Serikali za Mitaa katika sehemu kubwa nchini umeshindwa kufanyika kwa sababu mbalimbali,zikiwemo za kutofikishwa kwa Vifaa vya kupigia kura Vituoni.

Wakati maeneo mengine uchaguzi huo licha ya kufanyika ,umetawaliwa na Vurugu ambazo baadhi ya vurugu hizo zimetokana na utaratibu mbovu uliopo katika kituo husika.

Pamoja na hayo Wananchi walio wengi wameilalamikia Serikali kwa kushindwa kuweka utaratibu mzuri wa kupiga kura hivyo wananchi wanaamini kutakuwa na hujma ndani yake.

Comments are closed.