CRISTIANO RONALDO ATWAA TUZO YA MCHEZAJI WA ULIMWENGU

CRISTIANO RONALDO ATWAA TUZO YA MCHEZAJI WA ULIMWENGU

Like
439
0
Tuesday, 30 December 2014
Slider

Nahodha wa timu ya taifa ta Ureno na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo amefanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji wa ulimwengu (Globe Soccer Award) huko nchini Dubai.

Ronaldo amepata tuzo hiyo mbele ya wachezaji mbalimbali kama Messi, Neuer ambao ndio wapinzani wake wakubwa katika tuzo inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka duniani ballon d’Or inayotarajiwa kutolewa tarehe 12 januari 2015.

RR

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya utoaji wa tuzo hizo, Ronaldo amesema anashukuru kwa kushinda tuzo hiyo na anamatumaini makubwa itakuwa ni kichocheo cha yeye kushinda ballon d’Or kwa mara ya pili mfululizo baada ya kuitwaa januari mwaka huu.

Cristiano amekuwa na msimu mzuri kwa kufanikiwa kuvunja rekodi mbalimbali huku akiiongoza klabu ya Real Madrid kushinda mechi takribani 22 mfululizo huku akiwa anaongoza kwa ufungaji wa magoli ndani ya ligi kuu nchini Hispania.

Comments are closed.