ALIEKUWA KOCHA WA STOKE CITY NA CRYSTAL PALACE YUPO MBIONI KUSAINI NA WEST BROMWHICH ALBION

ALIEKUWA KOCHA WA STOKE CITY NA CRYSTAL PALACE YUPO MBIONI KUSAINI NA WEST BROMWHICH ALBION

Like
296
0
Wednesday, 31 December 2014
Slider

Aliyekuwa kocha wa klabu ya Stoke City na Crystal Palace yu mbioni kusaini mkataba wa kukinoa kikosi cha klabu ya West Bromwhich Albion kwa kuziba nafasi ilioachwa wazi na aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Alan Irvine.

Pulis ambaye ni mshindi wa tuzo ya ya kocha bora msimu uliopita amekubali kujiunga na klabu ya West Brom na kuitosa Newcastle baada ya mazungumzo ya kina baina yake na wamiliki wa pande zote mbili.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 56 amesema hakuwa teyari kujiunga na Newcastle kwasababu mmiliki wa klabu hiyo, Mike Ashley hayupo teyari kumuachia kocha afanye maamuzi katika masuala ya usajili wa wachezaji.

Pulis ataungana na aliyekuwa kocha msaidizi wakati yupo Stoke City, David Kemp huku mechi yake ya kwanza inatarajiwa kuwa siku ya mwaka mpya dhidi ya wagonga nyundo wa London klabu ya West Ham United.

Comments are closed.