DAKTARI WA CHELSEA ABWAGA MANYANGA

DAKTARI WA CHELSEA ABWAGA MANYANGA

Like
213
0
Wednesday, 23 September 2015
Slider

Daktari wa klabu ya Chelsea ya nchini England Eva Carneiro ameamua kuondoka katika klabu hiyo wiki sita baada ya kukwaruzana na meneja wa timu Jose Mourinho.

Carneiro aliingiliwa katika majukumu yake baada ya Mourinho kusema kuwa benchi lake la matibabu lilikuwa na watu wasiojua majukumu yao kwa kumtibu hovyo Eden Hazard wakati wa sare ya 2-2 na Swansea tarehe 8 Agosti.

Chelsea ilimuomba Carneiro mwenye miaka 42 kurejea kazini lakini alikataa na kwa sasa analishughulikia suala hilo kisheria zaidi.

Chama cha Soka nchini humo FA kinafuatilia malalamiko kwamba Mourinho alitumia lugha ya matusi au kijinsia juu yake.

Chelsea wanasema hawana maoni juu ya masuala ya ndani ya Utumishi.

Mwenyekiti wa Ushirikishwaji wa Bodi ya Ushauri ya FA Heather Rabbatts, ameelezea kusikitishwa kwake juu ya kuondoka kwa Carneiro.

Comments are closed.