DESIRE LUZINDA AANDAMWA NA MADENI

DESIRE LUZINDA AANDAMWA NA MADENI

Like
309
0
Tuesday, 06 January 2015
Entertanment

Octoba 21 mwimbaji kutoka Uganda Desire Luzinda alikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa kushindwa kulipa deni la shilingi milioni 21 za Uganda alilokopa kwa mfanyabiashara mmoja nnchini humo alizozitumia kufanyia party yake ya All White affair concert.

Mwimbaji huyo ambae aliekuwa akiandamwa na skendo ya picha zake za utupu kuvuja alipata msaada kutoka kwa rafiki yake aliemlipia milioni kumi na kuahidi kumalizia deni hilo hapo baadae.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Uganda kwa sasa mkali huyo anakabiliwa na deni linguine lipatalo shilingi Milioni hamsini za Ug. Amabapo Desire alimuahidi mfanyabiashara anaemdai aliefahamika kwa jina la Jimmy kuwa atamlipa kwa awamu, Jimmy amedai kuwa amekuwa na wakati mgumu kukutana na Desire kufuatia ulinzi mkubwa anaouweka anapotoka lakini pia hata akienda kwao hukutana tu na mama wa msanii huyo

Kwa upande wa Desire amedai kuwa matatizo ya kifedha yanawakuta watu wengi lakini pia huwa anamiliki dola za kutosha hivyo hawezi kukimbia na hizo milioni hamsini hivyo atalilipa deni hilo

Comments are closed.