DK SHEIN AAHIDI KUJENGA HOSPITALI YA KISASA BINGUNI ZANZIBAR

DK SHEIN AAHIDI KUJENGA HOSPITALI YA KISASA BINGUNI ZANZIBAR

Like
347
0
Tuesday, 22 September 2015
Local News

MGOMBEA wa nafasi ya urais wa zanzibar kupitia chama cha mapinduzi –CCM- dokta Ali Mohamed Shein ameahidi kujengwa kwa hospitali mpya ya kisasa eneo la binguni wilaya ya kati mkoa wa kusini Unguja.

Dokta Shein ameyasema hayo katika mkutano wa kampeni ya uchaguzi wa chama hicho uliofanyika bungi miembe mingi wilaya ya kati, mkoa wa kusini unguja na kuhudhuriwa na maelfu ya wananchi.

Katika mkutano huo amesema kuwa hospitali hiyo itakuwa kubwa na ya kisasa, ambayo itakuwa na idara mbalimbali zikiwemo idara ya upasuaji wa moyo, na saratani kwa lengo la kupunguza mzigo katika hospitali ya mnazi mmoja.

Comments are closed.