FEDHA ZA MKESHA WA KUOMBEA AMANI KUTUMIKA KUSAIDIA WATU WENYE MAHITAJI HASA AFYA YA MAMA NA MTOTO

FEDHA ZA MKESHA WA KUOMBEA AMANI KUTUMIKA KUSAIDIA WATU WENYE MAHITAJI HASA AFYA YA MAMA NA MTOTO

Like
164
0
Tuesday, 29 December 2015
Local News

IMEELEZWA kuwa Fedha zitakazopatikana katika Tamasha la mkesha wa kuombea amani  nchini zitatumika kuwasaidia watu wenye mahitaji  hasa afya ya mama na mtoto.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti  wa Jumuiya  wa Makanisa ya Pentekoste , ambaye pia ni Askofu wa huduma ya Tanzania Fellowship TFC,  Askofu  Godfrey  Malassy  alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.

 

Askofu Malassy amesema kwamba, fedha zitakazopatikana katika tamasha hilo zitanunua vifaa vinavyotumia nishati ya jua ili kuwasaidi wamama wajawazito na watoto wanaozaliwa.

Comments are closed.