FERGUSON: MEYA ATANGAZA KUWACHUKULIA HATUA POLISI DHIDI YA VITENDO VYA UBAGUZI WA RANGI

FERGUSON: MEYA ATANGAZA KUWACHUKULIA HATUA POLISI DHIDI YA VITENDO VYA UBAGUZI WA RANGI

Like
156
0
Thursday, 05 March 2015
Global News

MEYA wa mji wa Ferguson, jimboni Missouri, ametangaza hatua zitakazochukuliwa kufuatia ripoti iliyoonyesha ushahidi dhidi ya polisi wa mjini humo kujihusisha na vitendo vya ubaguzi wa rangi.

Meya JAMES KNOWLES amesema mwajiriwa mmoja toka Idara ya Polisi amefukuzwa kazi na wengine wawili wamelazimishwa kwenda likizo baada ya kushutumiwa kutuma barua pepe yenye ujumbe wa kibaguzi.

KNOWLES amewaambia Waandishi wa Habari kuwa Idara itaongeza namba ya Maafisa wasio wazungu na kujikita katikamafunzo.

Comments are closed.