GEITA GOLD MINE YAUNGANA NA WATANZANIA KUADHIMISHA SIKU YA UKIMWI DUNIANI

GEITA GOLD MINE YAUNGANA NA WATANZANIA KUADHIMISHA SIKU YA UKIMWI DUNIANI

Like
196
0
Tuesday, 01 December 2015
Local News

KAMPUNI ya Uchimbaji madini ya Geita Gold Mine leo imeungana na Watanzania kuadhimisha siku ya ukimwi duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Disemba mosi kila mwaka.

Akizungumza na Wanahabari Jijini Dar es salaam Makamu wa Rais wa kampuni hiyo Simon Shayo amesema kuwa nchi nyingi zinazoendelea  zimekuwa hazipati fedha nyingi kama ilivyokuwa mwanzoni kutoka  kwa Mataifa makubwa hali inayosababisha utoaji huduma kuwa mgumu.

Aidha Shayo ameongeza kuwa ndoto ya mkakati wa kutoa Elimu juu ya ugonjwa huo ni kufikia mahali ambapo viwango vya maaumbikizi vitashuka kwa kiwango kikubwa.

Comments are closed.