GHANA YATANGAZA SIKU TATU ZA MAOMBOLEZO KUFUATIA VIFO VYA WATU 150

GHANA YATANGAZA SIKU TATU ZA MAOMBOLEZO KUFUATIA VIFO VYA WATU 150

Like
339
0
Friday, 05 June 2015
Global News

GHANA imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo vya watu mia na hamsini vilivyotokana na mafuriko na mlipuko kwenye kituo kimoja cha mafuta.

 

Mlipuko huo ulitokea hapo jana wakati mamia ya watu walipokuwa wamejihifadhi katika kituo hicho cha mafuta kutokana na mvua kubwa zinazonyesha.

 

Rais wa Ghana,John Mahama amesema janga kama hilo halitajirudia tena. Rais Mahama amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mji mkuu ,Accra alipotembelea eneo la tukio.

baadhi ya picha za ajali ya moto Ghana

150604093627_ghana_fire_640x360_bbc_nocredit

 

 

150604092839_ghana_floods_accar_640x360_bbc_nocredit

 

 

150604131908_ghana_fire_640x360_epa

 

Comments are closed.