HALMASHAURI YA MANISPAA YA KINONDONI YAJENGA MAABARA 138

HALMASHAURI YA MANISPAA YA KINONDONI YAJENGA MAABARA 138

Like
279
0
Friday, 12 December 2014
Local News

 

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kinondoni imefanikiwa kujenga maabara 138 ikiwa ni agizo la Rais JAKAYA KIKWETE la kutaka kila shule za Kata ziwe na Maabara.

Hayo yamebainishwa jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Mhandisi MUSA NATTY wakati wa hafla ya kukabidhi vyeti kwa wafanyakazi waliofanya vizuri wakiwamo wasimamizi wa Maabara hizo.

Mhandisi NATTY ameeleza kuwa kwa kiasi kikubwa wametimiza agizo la rais kwani awali walikuwa na maabara 12 na vyumba 126 hivyo kufanya idadi ya maabara kufikia 138 kwa kipindi cha miezi miwili.

Comments are closed.