HAMILTON ATWAA TAJI LA JAPAN GP

HAMILTON ATWAA TAJI LA JAPAN GP

Like
242
0
Monday, 28 September 2015
Slider

Dereva wa magari yaendayo kasi Lewis Hamilton ameshinda michuano ya Suzuki na kutwaa taji la 41 katika mchezo huo.

Dereva huyu wa timu Mercedes, alishinda taji hilo na kumfikia mkongwe wa michuano ya Fomula 1 Mbrazili Ayrton Senna.

Hamilton alimzidi kwa alama 48 dereva mwenzake wa timu ya Mercedes, Nico Rosberg, katika mbio za michuano hiyo ya Grand prix.

Kukiwa kumesalia mbio tano Hamilton, anashikilia alama 48 zaidi ya Rosberg, huku akionekana na uwezo wa kushinda taji lingine la tatu la Fomula 1.

Comments are closed.