HUDUMA YA USAFIRI YAREJEA RELI YA KATI

HUDUMA YA USAFIRI YAREJEA RELI YA KATI

Like
229
0
Monday, 14 March 2016
Local News

HUDUMA ya usafiri wa reli ya Kati iliyokuwa imesimama kwa takribani miezi miwili sasa imerejea kufuatia kukamilika kwa ukarabati wa reli hiyo katika eneo la kidete wilayani kilosa, mkoani Morogoro.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amesema hayo baada ya kukagua na kuridhika na ukarabati uliofanywa katika maeneo ya Magulu, Munisagara, Mzaganza na kidete Wilayani Kilosa.

 

 

Comments are closed.