ICTR KUTOA HUKUMU YA MWISHO

ICTR KUTOA HUKUMU YA MWISHO

Like
185
0
Monday, 14 December 2015
Local News

MAHAKAMA ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) iliyokuwa ikishughulikia kesi za mauaji yaliyotokea miaka 20 iliyopita leo itatoa hukumu yake ya mwisho kabla ya kufungwa rasmi.

 

Hukumu hiyo itakuwa dhidi ya watuhumiwa Pauline Nyiramasu ambaye ni waziri wa zamani wa Maendeleo ya wanawake nchini Rwanda na mtoto wake ambaye wote wamekana mashtaka yanayowakabili.

 

Mahakama hiyo ambayo imekuwa nchini katika mji wa Arusha ilikuwa ikisikiliza kesi za watuhumiwa wa mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994.

Comments are closed.