JAMII IMETAKIWA KULINDA AMANI YA NCHI

JAMII IMETAKIWA KULINDA AMANI YA NCHI

Like
183
0
Monday, 24 August 2015
Local News

JUKWAA la Tiba asili Tanzania limewaasa wananchi kuithamini na kuendeleza Amani iliyopo kwa kuepuka kujihusisha na vishawishi vitakavyosababisha kuvunjika kwa Amani.

 

Wito huo umetolewa Jijini Dar es salaam na mwenyekiti wa Jukwaa hilo Bonaventure Mwalongo wakati akizungumza na kituo hiki juu ya umuhimu kwa watanzania kushiriki katika kuilinda na kuitetea Amani.

 

Mwalongo amebainisha kuwa ni muda muafaka sasa kwa kila mtu bila kujali itikadi ya chama, dini au kabila kushirikiana kwa pamoja katika kila suala muhimu na lenye manufaa kwa Taifa pamoja na kupiga vita vitendo vya uvunjifu wa Amani.

 

Comments are closed.