JESHI LA KENYA LATUHUMIWA KUFANYA BIASHARA SOMALIA

JESHI LA KENYA LATUHUMIWA KUFANYA BIASHARA SOMALIA

Like
238
0
Thursday, 12 November 2015
Global News

JESHI la Kenya limetuhumiwa kujihusisha na shughuli mbalimbali kinyume na malengo ikiwemo kufanya biashara badala ya kufanya kazi zinazowahusu nchini Somalia.

Taasisi ya Waandishi wa habari Wanaopigania haki imelituhumu Jeshi hilo kujiingiza katika masuala mbalimbali ya kibiashara yanayowaletea faida na kuacha kazi ya iliyowapeleka ya kulinda Amani.

Hata hivyo Taasisi hiyo imewalaumu baadhi ya maofisa wa jeshi hilo kushirikiana katika biashara haramu na wapiganaji wa Al Shabaab jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Comments are closed.