KASHFA YA UFISADI: SEPP BLATTER NA MICHEL PLATINI WAFUNGIWA MIAKA 8

KASHFA YA UFISADI: SEPP BLATTER NA MICHEL PLATINI WAFUNGIWA MIAKA 8

Like
229
0
Monday, 21 December 2015
Slider

Maafisa wawili wakuu zaidi katika usimamizi wa kandanda duniani rais Sepp Blatter na mwenyekiti wa shirikisho la soka barani ulaya UEFA Michel Platini, wamepigwa marufuku ya miaka 8 ya kutoshiriki kwa vyovyote maswala ya soka kufuatia uchunguzi wa kimaadili.

Wamepatikana na hatia ya ukiukaji wa maswala mbalimbali kama vile kashfa ya dola milioni mbili malipo yasiyo rasmi ambazo zilikabidhiwa Patini mwaka 2011.

Maafisa hao wawili wanasisitiza kutofanya makosa yoyote.

Marufuku hiyo inaanza kutekelezwa mara moja.

Rais huyo wa Fifa tangu mwaka 1998, Bwana Blatter, mwenye umri wa miaka 79, tayari ametangaza kujiondoa katika kinyanganyiro cha kumtafuta rais mpya wakati wa uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo mwezi Februari mwakani.

Naye nahodha wa zamani wa Ufaransa Platini, mwenye umri wa miaka 60, na ambaye alionekana kama kiongozi wa baadaye wa shirikisho hilo, amekuwa akipigiwa upatu wa kuchukua mahala pa Blatter katika uchaguzi mkuu unaopangiwa kufanyika Februari mwakani.

Bingwa huyo mara tatu wa mchezaji bora wa mwaka wa bara Ulaya na nahodha wa zamani wa Ufaransa, amekuwa Rais wa UEFA tangu mwaka 2007.

Comments are closed.