KERRY KUWAKILISHA MAREKANI KUZUNGUMZIA NYUKLIA IRAN

KERRY KUWAKILISHA MAREKANI KUZUNGUMZIA NYUKLIA IRAN

Like
245
0
Friday, 21 November 2014
Global News

WAZIRI WA MAMBO ya Nje wa Marekani, JOHN KERRY, amewasili mjini Vienna, Austria, kushiriki Kongamano la Mataifa Sita yenye nguvu Duniani na Iran juu ya mpango wa nyuklia wa Iran.

Msemaji wa Wizara hiyo, JENIFFER PSAKI, amesema bado haijafahamika lini Waziri huyo ataondoka Vienna kurejea Washington, huku timu za wapatanishi zikipigania kupatikana kwa makubaliano na Iran kabla ya muda wa mwisho siku ya Jumatatu ijayo.

Taarifa zaidi zimeleeza kuwa ikiwa makubaliano hayo yatafikiwa, mkwamo wa Miaka 12 kwenye mpango wa Atomiki wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran utakwamuliwa.

 

Comments are closed.