KOMAA CONCERT KUFANYIKA JUMAMOSI TAREHE 30 WIKI HII

KOMAA CONCERT KUFANYIKA JUMAMOSI TAREHE 30 WIKI HII

Like
481
0
Monday, 25 May 2015
Entertanment

Tamasha kubwa la kuadhimisha miaka kumi na sita ya msanii JUMA NATURE  maarufu kama kiroboto pamoja na hitimisho la sherehe za mwaka mmoja za 93.7 EFM linalofahamika kama KOMAA CONCERT kwa mara ya kwanza litafanyika rasmi  jumamosi hii ya  tarehe 30 mwezi mei katika ukumbi wa Dar Alive –Mbagala,  kuanzia saa kumi na mbili jioni.

 

Tamasha hili limeandaliwa na Juma nature akishirikiana na EFM kwa lengo la kuwaburudisha Mashabiki wa juma nature na wasikiliazaji wa 93.7 EFM ikiwa ni sehemu ya kuwashukuru mashabiki kwa ushirikiano wao kwa miaka kumi na sita ya muziki tangu kuanza msanii huyo  Juma Nature aingie kwenye game ya Muziki nchini Tanzania.

 

Aidha, mashabiki watapata burudani kutoka kwa kiroboto  ambaye atatumia dakika 180 akiwa jukwaani kuhakikisha anakonga nyoyo za mashabiki wake ambapo ataimba nyimbo zake zote kali zilizofanya vizuri na kusindikizwa na wasanii kibao.

 

Miongoni mwa wasanii hao ni pamoja na  Profesa Jay, Shetta, Snura, Makomando, Msagasumu na wengine wengi.

 

Tunatoa wito kwa mashabiki wote wa juma nature , Efm Radio, wadau na wengine kujitokeza kwa wingi siku ya tamasha hili ili kupata burudani hii ya kihistoria ambapo kiingilio kitakuwa ni shilingi 7,000 tu.

 

Tunaamini Juma nature ni msanii mwenye kipaji kikubwa na aliyewahamasisha wasanii kibao kuingia katika muziki huu wa kizazi kipya hivyo anastahili kupewa heshima kubwa kwa mchango wake mkubwa katika kukuza muziki wa kizazi kipya.

 

Lakini kwa Efm huyu ni msanii wa Kwanza itaendelea kufanya hivyo kwa wasanii wengine kwakuwa kwetu sisi tunaamini

Muziki unaongea.

DU7C5559

DU7C5558

DU7C5556

DU7C5642

DU7C5600

DU7C5608

DU7C5568

DU7C5576

DU7C5590

DU7C5594

DU7C5597

DU7C5627

DU7C5566

IMETOLEWA NA,

DENIS SSEBO,

MENEJA MAWASILIANO NA MAMBO YA SHERIA WA EFM.

Comments are closed.