KOREA KASKAZINI YATANGAZA KUFANYA JARIBIO LA NYUKLIA

KOREA KASKAZINI YATANGAZA KUFANYA JARIBIO LA NYUKLIA

Like
231
0
Tuesday, 15 March 2016
Global News

KIONGOZI wa Korea Kaskazini Kim Jong-un ametangaza kwamba Taifa hilo litafanya majaribio ya silaha zake za nyuklia na makombora ya masafa marefu hivi karibuni.

Kim Jong-un ametoa Tangazo lake alipokuwa akiongoza maonesho ya teknolojia ambayo inahitajika kuwezesha kombora lenye kilipuzi cha nyuklia kuingia tena ardhini baada ya kurushwa anga za juu.

Shirika hilo limemnukuu kiongozi huyo akisema kuwa majaribio hayo yatafanyika na yataisaidia Korea Kaskazini kujiimarisha katika utekelezaji wa mashambulio ya makombora.

Comments are closed.