MAJIBU YA DIAMOND KWENYE KIPINDI CHA GENGE KUPITIA 93.7EFM LEO

MAJIBU YA DIAMOND KWENYE KIPINDI CHA GENGE KUPITIA 93.7EFM LEO

Like
614
0
Thursday, 20 November 2014
Entertanment

Tofauti kati ya waandaji wa video za bongo na wa nje ni ?

upatikanaji wa vitu vya kuijenga Script pindi vinapohitajika mfano unapohitaji nyumba kama hekaru, uwezo wa kuifikisha nyimbo kwenye vituo vya tv vya nje mf. Trace, Mtv, Channel o n.k

lakini pia Diamond alidai kuwa waandaji wa ndani wanamikwala Mingi katika kuruhusu mawazo ya msanii wakati wa uandaaji wa Video

alipouulizwa kuhusu mafanikio ya wasanii wa Nigeria yanakuja kufuatia kuwa wengi kwenye ramani ya muziki wa Afrika Diamond alisema kwa kulitambua hilo hivi sasa ameenza kuwaunganisha wasanii wa ndani kufanya nyimbo pamoja na wasanii wa nje mf. Sheta na K ceee wa Nigeria lakini pia Fid Q ambae amemuita mfalme wa hiphop na Sarkodie.

Diamond pia aliulizwa kama anadhani yeye ndie msanii mwenye uwezo wa kuimba kuliko wasanii wengine kutoka Tanzania alijibu kuwa Juhudi zake ndio mafanikio yake na wala hadhani kuwa anauwezo kuliko watu wote.

Pia alizungumzia juu ya mafanikio aliyoyapata kwenye ngoma ya mdogomdogo kwenye moja ya Tuzo zilizofanywa huko nje zikishindanisha nyimbo kama Aye ya Davido na kupenya kutoka na ushindi wa kuwa nyimbo bora yenye vionjo vya Afrika 

10378252_833977959957353_2677925388952221456_n

sehemu ya video ambayo huenda ikatoka leo

 

 

 

Comments are closed.