MALAYSIAN GRAND PRIX: SEBASTIAN VETTEL AMBWAGA LEWIS HAMILTON

MALAYSIAN GRAND PRIX: SEBASTIAN VETTEL AMBWAGA LEWIS HAMILTON

Like
318
0
Monday, 30 March 2015
Slider

Dereva wa mbio za magari wa timu ya Ferrari Sebastian Vettel raia wa Ujeruamani ameibuka na ushindi kwenye mashindano ya Malaysian Grand Prix baada ya kumbwaga Lewis Hamilton wa timu ya Mercedes.

Ushindi huo wa Vettel kwenye michuano hiyo ni wa kwanza katika mashindano hayo akiwa na timu ya Ferrari Ushindi wa mjerumani huyo umemfanya kuwa ndiye dereva mwenye mafanikio makubwa katika eneo la Sepang akiwa na mataji manne

Katika pambano hilo lililokuwa na ushindani mkali Hamilton alifanikiwa kushika nafasi ya pili baada ya kupitia misukosuko kufuatia tairi la gari lake kuharibika kutokana na joto kwenye ukanda huo wa kitropic huku nafasi ya tatu ikienda kwa Nico Rosberg.

SEB4 SEB3 SEB2

Comments are closed.