MAN CITY YALAZWA 2-1 NA CSKA MOSKVA HUKO ETIHAD

MAN CITY YALAZWA 2-1 NA CSKA MOSKVA HUKO ETIHAD

Like
243
0
Thursday, 06 November 2014
Slider

Klabu ya Manchester City imejikuta katika wakati mgumu baada ya kupokea kipigo cha magoli mawili kwa moja dhidi ya CSKA Moskva ndani ya uwanja wao wa nyumbani Etihad,

Magoli mawili ya Seydou Doumbia mnamo dakika ya pili ya mchezo huo na lile jengine mnamo dakika ya 34 yalitosha kuwaangamiza mabingwa hao watetezi wa ligi kuu nchini England huku goli lao la kufutia machozi likifungwa na Yaya Toure ambae baadae alionyeshwa kadi nyekundu.

Toure alipewa kadi nyekundu dakika ya 81 huku City ikiwa teyari ishampoteza kiungo wa kiBrazil Fernandinho aliyelimwa kadi nyekundu dakika ya 70 hivyo kumaliza mchezo huo wakiwa 9 tu uwanjani.

Matokeo hayo yameshuhudia City ikitupwa mpaka mkiani mwa kundi E ikiwa na jumla ya alama 2 hivyo kuwalazimu kushinda michezo miwili iliyobakia dhidi ya Bayern Munich mwenye alama 12 na AS Roma mwenye alama 4.

Doumbia_3097231b

Comments are closed.