MANISPAA YA ILALA YALALAMIKIWA KUSHINDWA KUREKEBISHA UCHAKAVU WA MIUNDOMBINU YA MAJITAKA

MANISPAA YA ILALA YALALAMIKIWA KUSHINDWA KUREKEBISHA UCHAKAVU WA MIUNDOMBINU YA MAJITAKA

Like
233
0
Wednesday, 02 December 2015
Local News

UONGOZI wa Muungano wa Wafanyabiashara wa Masoko Mkoa wa Dar es salaam MUMADA waliopo Soko la Kibasila wameilalamikia Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kwa kushindwa kurekibisha uchakavu wa miundombinu ya majitaka, mazingira pamoja na majengo ya soko hilo la Kibasila licha ya Manispaa hiyo kukusanya ushuru wa kutosha kuboresha hali ya mazingira katika soko hilo.

 

Akizungumza na Efm  jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa Muungano wa Wafanyabiashara Masoko kanda ya Ilala Issa Malisa amesema uongozi hauko tayari  kuona kampuni binafsi zinapewa tenda ya kuchukua ushuru na kukusanya taka katika eneo hilo wakati Wafanyabiashara wa Soko hilo wanaweza kufanya kazi hiyo.

 

Comments are closed.