MANNY PACQUIAO: MAYWEATHER JNR ATATANGAZA PAMBANO LETU

MANNY PACQUIAO: MAYWEATHER JNR ATATANGAZA PAMBANO LETU

Like
263
0
Monday, 16 February 2015
Slider

Floyd Mayweather Jnr ameikana taarifa inayodai kuwa mpinzani wake Manny Pacquiao ametilia saini mkataba wa kupambana nae huko Las Vegas ifikapo tarehe mbili mwezi wa tano ila Mayweather ameeleza kwamba anamatumaini juu ya pambano hilo kufanyika.

Mbabe huyo kutoka nchini Marekani ameonyesha utayari wake juu ya pambano hilo na kusisitiza kwamba bado hakuna makubaliano yoyote yakimaandishi yaliyosainiwa kuthibisha kufanyika kwa pambano hilo.

Mayweather aliyasema hayo alipokuwa kwenye NBA All-Star Game katika viwanja vya Madison Square Garden siku ya jumapili.

 Pacquiao pia kwa upande wake mwishoni mwa wiki alinukuliwa akisema kuwa Mayweather ndie atakaetangaza pambano hilo kama makubaliano ya mwisho yatafikiwa.

Pacquiao na Mayweather walikutana Miami nchini Marekani mwezi uliopita wakati wakifuatilia mpambano wa kikapu kisha kubadilishana namba

  may3may

 

http://youtu.be/9kq0eVg9LuY

Comments are closed.