MARUBANI WA SHIRIKA LA NDEGE LA UJERUMANI LUFTHANSA WATANGAZA KUENDELEA NA MGOMO LEO

MARUBANI WA SHIRIKA LA NDEGE LA UJERUMANI LUFTHANSA WATANGAZA KUENDELEA NA MGOMO LEO

Like
361
0
Friday, 20 March 2015
Global News

MARUBANI wa Shirika la ndege la Ujerumani Lufthansa wametangaza kwamba wataendelea na mgomo wao leo mgomo ambao tayari umewaathiri maelfu ya abiria na kushuhudia kufutwa kwa mamia ya safari kutokana na mzozo juu ya mpango wa malipo ya kustaafu.

Msemaji wa Shirika la ndege la Lufthansa amesema nusu ya safari 1,400 za shirika hilo za ndani na zile za Ulaya kuingia na kuondoka Frankfurt na Munich zimefutwa hapo na kuathiri abiria 80,000.

Mgomo huo wa siku moja awali ulikuwa umepangwa kuendelea hadi March 19 ambapo ulikuwa ulenge safari za masafa marefu na ndege za mizigo.

GERMANYY

Comments are closed.